Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Wednesday, December 31, 2014

MTUHUMIWA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI MAHAKAMANI

Mtuhumiwa wa kesi ya madawa ya kulevya leo majira ya asubuhi aliuwawa kwa kupigwa risasi na askari magereza baada ya kushindwa katika jaribio la kutoka kutoroka. Mtuhumiwa huyo akiwa amefikishwa mahakamani kutoka mahabusu aliwakimbia walizi hao na kuparamia ukuta wa mahakama akiwa na lengo la kutoroka kabla ya kuuwawa na askari hao waliokuwepo mahakamani hapo. Picha zaidi na wadau wetu. Baadhi ya picha kwa hisani ya Global Publishers

Sunday, December 7, 2014

MDAU WENU NILIPOTEMBELEA MOJA YA MAAJABU 7 YA DUNIA KASRI YA TAJ MAHAL NCHINI INDIA

Mdau wenu nilipokuwa dhiarani nchini India, moja ya maeneo niliyofanikiwa kuyatembelea ilikuwa ni pamoja na makumbusho ya Kasir ya mfalme wa zamani aliyewahi kutawala nchini India. Kivutio kikubwa katika kasri hiyo kubwa iliyosheheni vito vya thamani ni makaburi mawili makubwa ya mke wa tatu wa mfalme huyo pamoja na kaburi la mwanae. Inasemekana mfalme huyo aliyejaliwa kuwa na wake watatu alimpenda sana mke wake wa tatu na hata kuamua kumjengea kasri hiyo ili atakapokufa mwili wake uhifadhiwe humo. Kasri hiyo iliyojengwa na watumishi wapatao 1400 ilikamilika katika kipindi cha miaka 4 na kila mfanyakazi aliyehusika katika ujenzi huo baada ya kumalizika kwa ujenzi mfalme aliamuru akatwe kiganja cha mkono wa kulia kusudi wasiweze kujenga mfano wa kasri hiyo popote hapa duniani. Kasri hii kubwa nchini India ni moja kati ya maajabu saba ya Dunia.
Sanamu ya mfano wa Kasri ya Taj Mahal
Raia mbalimbali wa Kigeni wakiangalia moja ya maajab ya dunia ya Taj Mahal nchin India
 
Mdau nikiwa mbele ya Kasri ya Taj Mahal 
Kila anaefika mahali hapa anapenda kupiga picha ya muonekano huu
 

Thursday, November 20, 2014

AJALI YAFUNGA BARABARA MIKUMI

Leo ama una safari ya kwenda Iringa, Mbeya au kama unapokwenda utapita mikumi basi sitisha safari kwani njia imefungwa tangu saa mbili asubuhi. Kuna lory linawaka moto mpaka sasa. Lilikuwa limebeba lami so lami bado inawaka na imesambaa sehemu kubwa.

Friday, November 14, 2014

BREAKING NEWS!! MACHINGA COMPLEX YAUNGUA MOTO

Soko kubwa na la kisasa lililopo maenea ya Ilala karibu na uwanja wa mpira wa Karume maarufu kama Machinga Complex linalomolikiwa na Manispaa ya Jiji la Ilala katika Mkoa wa Dar-es-Salaam, leo limeteketea vibaya na moto ulioanzia katika ghorofa ya pili. Mpaka tunapata habari hii chanzo cha moto huo kilikuwa hakijajulikana.

Thursday, November 13, 2014

MAJIBU YA SMS KWA MPENZI WAKO VYENYE VIASHILIA VYA KUOMBWA HELA

Ukiona umemtumia mpenzi wako/mchumba wako/mchepuko wako/mke wako au hata rafiki wa kike wakati mwingine SMS ya kawaida tu kwaajili ya kumsalimia lakini yeye akakujibu moja kati ya majibu yafuatayo, tafadhali sana usiendelee kuchat nae maana kinachofuata hapo ni majanga tu.

KWA MFANO: 
1. Ukimtumia sms ''Mambo mpenzi wangu?'' akikujibu ''mambo mabaya'', usimuulize kwanini mambo mabaya, ukimuuliza atakwambia kuwa ''sina hela dear''

2. Ukimtumia sms ''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' akikujibu ''maisha magumu hubby wangu we acha tu'' usimuulize kwanini, ukimuuliza kwanini atakwambia ''nimefulia mwenzio kama nini sijui''

3. Ukimtumia sms ''Mbona kimya sana mchumba wangu, umenitupa kiasi hicho'' akikujibu ''sijakutupa wangu yaani mambo hata hayaendi'' usimuulize kwanini mambo hayaendi, ukimuuliza atakwambia kuwa ''yaani sina kitu mpenzi wangu, simu ilikuwa haina hata hela ya kubeep''

4. Au ukiona mwanamke anaanza kwa kukwambia nikwambie kitu? We mkatalie kiutani utani tu, mwambie usiniambie, hata akikomaa vipi akwambie mwambie sitaki uniambie huku unafanya kama utani lakini moyoni unakuwa upo serious.

Ni mara chache sana mwanamke akikwambia kuwa mambo mabaya, maisha magumu au mambo hayaendi huwa na matatizo mengine kama kuumwa, misiba.... n.k lakini THE REST ni wapigaji mizinga tu. Akikwambia maisha magumu mjibu ''pole wangu, mambo mengine vipi?''

Ukipewa majibu kama hayo, chagua moja, either usiendelee kuchat nae mpaka badae kidogo au mbadilishie maada ili kukwepa huo mzinga ambao unakuja mbele yako. ��������

Thursday, November 6, 2014

MWANAMKE ATUPA KITOTO KICHANGA CHOONI

IRINGA,
Mama mmoja mjini Iringa aamua kumtupa mtoto wake chooni mara baada ya kumzaa nyumbani.
Mtoto huyo wa kiume aliezaliwa tarehe 4/11/2014 majira ya jioni na mama huyo na kuamua kumdumbukiza chooni ambapo kisa mpaka sasa anamkwepa mumewe aliyepo safarin asijue kuwa amepata mimba na kuzaa.
Hata hivyo chanzo cha habari kinasema kuwa, mama huyo kwa jina la magdalena limano (32) mkazi wa Iringa anatabia ya kumdanganya mumewe na kutoka na mabwana wengine pindi mumewe akiwa safarini kikazi.
Mtoto huyo aliyetupwa choon majira ya jioni mara baada ya kuzaliwa na kukutwa asubuhi ya tarehe 5/11 asubuhi akiwa analia ndani ya choo na majirani na kutoa taarifa.
Mpaka sasa mtoto ni mzima wa afya na yupo katika uangalizi mzuri wa hospitali huku mama akishikiliwa na jeshi la polisi akisubiri kupandishwa mahakamani.
Picha zifuatayo linaonyesha tukio kamili: Habari kwa hisani za mtandao wa kijamii Whatsapp.

 
 Kichanga kikisafishwa mara baada ya kuopolewa chooni...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi wa wakuu wapya wanne wa Mikoa, amewahamisha wengine sita na ameamua kuwa wengine watatu watapangiwa kazi nyingine.

Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jioni ya leo, Jumatano, Novemba 5, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa, Wakuu wapya wa Mikoa ni Bi. Halima Omari Dendego ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Dkt. Ibrahim Hamisi Msengi ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Bi. Amina Juma Masenza ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Bwana John Vianney Mongella ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Taarifa inasema kuwa kabla ya uteuzi wake Bi. Dendego alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dkt. Msengi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Bi. Masenza alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela na Bwana Mongella alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.

Taarifa hiyo inasema kuwa Wakuu hao wapya wa Mikoa wataapishwa kesho, Alhamisi, Novemba 6, 2014 saa saba mchana, Ikulu, Dar es Salaam.

Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ambao watapangiwa kazi nyingine ni Kanali (Mst) Fabian Massawe wa Kagera, Dkt. Christine Ishengoma wa Iringa na Kanali Joseph Simbakalia wa Mtwara.

Wakuu wa Mikoa ambao wamehamishwa vituo vya kazi ni Bwana Magesa S. Mulongo ambaye anakwenda Mkoa wa Mwanza kutoka Arusha, Dkt. Rehema Nchimbi ambaye anakwenda Mkoa wa Njombe kutoka Dodoma, Bwana Ludovick John Mwananzila anakwenda Tabora kutoka Lindi, Kepteni (Mst) Anseri Msangi anayekwenda Mkoa wa Mara kutoka Njombe na Mhandisi Everist Ndikilo ambaye anakwenda Arusha kutoka Mwanza.

Wengine waliohamishwa ni Luteni (Mst) Chiku A.S. Galawa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutoka Tanga, Dkt. Rajab Rutengwe ambaye anakwenda Mkoa wa Tanga kutoka Katavi, Bi Fatma Mwasa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kutoka Tabora na Bwana Magalula S. Magalula ambaye anahamishiwa Lindi kutoka Geita.

Taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ya Dar es Salaam, Kigoma, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,Morogoro, Pwani, Rukwa, Shinyanga, Ruvuma, Singida na Simiyu watabakia kwenye vituo vyao vya sasa.

Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi wa Wakuu wapya wa Wilaya, kuhamisha baadhi yao na kutengua uteuzi wa baadhi.

Taarifa kamili itatolewa na Waziri Mkuu baada ya kuwa wamepangiwa vituo vya kazi.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
05 Novemba,2014

Monday, November 3, 2014

MKUTANO WA MWALIMU NYERERE FOUNDATION KUHUSU KATIBA MPYA WAFANYIWA VURUGU

Taarifa ya tukio lililotokea ubungo plaza katika mkutano wa mwalimu Nyerere foundation: Mkutano ulifanyika kuanzia saa 1520hrs ukiwa chini ya uenyekiti wa Jaji Mstaafu mh. Joseph Sinde Warioba. Mkutano ulihudhuriwa na watu wa kada mbalimbali sambamba na itikadi tofauti za kisiasa. Mkutano ulirushwa moja kwa moja na ITV na maudhui yake kimtazamo ulilenga kuoanisha mapendekezo ya marekebisho ya Katiba ya tume ya Warioba na ile ya Mh. Sitta na tume yake. Baada ya Mh. Warioba kuelezea kwamba Muungano sio tunu ila ni urithi ndipo wakereketwa wa upande wa Mh. Sitta walipoinua mabango yasemayo pamoja na mambo mengine kwamba iweje wajadili mapendekezo ya katiba ya Mh. Sitta ambayo wao wameshaikubali? Baada ya mabango yale kuinuliwa yakazua tafrani ambapo walishauriwa kutoyainua kwa sababu haukuwa mkutano wa kisiasa na wakanyang'anywa na kuyachana ndipo vurugu/kashfa/matusi yakaanza kutolewa dhidi ya meza kuu. Hali hii ilisababisha kushikana, kusukumana na kurushiana viti. Katika tafrani hiyo mh. Warioba alipigwa kibao na Mh. Paulo Makonda- ambaye ni katibu wa UVCCM TAIFA. Mtuhumiwa huyu pamoja na wengine wanne wamekamatwa kwa mahojiano. Upelelezi unaendelea na juhudi za kuwapata wengine zinaendelea.

Sunday, November 2, 2014

SALAMU KUTOKA INDIA

Mdau wenu yupo matembezoni nchini India na ameamua kuleta kwa kifupi mambo anayokutana nayo kwa Muda wote atakaokuwepo nchini humo. Kaa tayari kupata yatakayojili.

Thursday, July 24, 2014

MKE WA MTU SUMU! JAMAA APIGWA NA SULULU KATIKA FUMANIZI

 
Samahani kwa picha zitakazofuatia katika habari hii. Jamaa mmoja mkoani Mara amenusurika kupoteza maisha baada ya kufumaniwa akiwa na mke wa mtu kitendo kilichopelekea kupigwa Sululu kichwani na mmiliki wa mke huyo. Habari zilizotufikia zimedai kuwa baada ya kupigwa na sululu hilo mtuumiwa aliwahishwa hospitali kwa matibabu. Hadi tunapata habari hizi hatukuwaeza kujua hali halisi ya mhanga huyo!

 
Sululu likiwa limenasa katika kichwa

Madaktari wakijitahidi kuokoa maisha ya mtuhumiwa

 
Baada ya kushonwa 

Wednesday, July 2, 2014

BREAKING NEWS!!! MAJAMBAZI YAFANYA JARIBIO LA KUTOROSHA WAFUNGWA

Habari za kuaminika zimeifikia blog hii leo mchana zikisema majambazi yasiyojulikana leo katika maeneo ya Mikocheni karibu na TMJ Hospital yaliirushia risasi basi lililokuwa limebeba wafungwa katika jitihada za kutaka kuwatorosha wafungwa. Hadi tunapata habari hizi ilikuwa haijulikani kama kuna yeyote aliyejeruhiwa au kupoteza maisha katika shambulio hilo. Hali kadharika haijulikani kama kuna mfungwa yeyote aliyetoroshwa hadi sasa!


 
 
 Watu wakiwa wamekusanyika kwenye tukio

 
Gari lililobeba wafungwa likiwa limevunjwa vioo
 

Thursday, June 26, 2014

MBUNGE WA KIGAMBONI DR. F. ANDUNGULILE AONGEA NA TANESCO KUHUSU KERO ZA UMEME

Mrejesho wa suala la umeme kwa maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kigamboni

Siku ya Jumatatu tarehe 23.06.2014 nilifanya mkutano na uongozi wa Tanesco ngazi ya Mkoa wa Temeke na Wilaya ya Kigamboni. Mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na:

Kukatika kwa mara kwa mara kwa umeme Umeme mdogo kwa baadhi ya maeneo Uunganishaji wa umeme kwa wateja wapyaMiradi mipya ya umeme kwa Jimbo la Kigamboni

1. KUKATIKA KWA MARA KWA UMEME JIMBO LA KIGAMBONI

Umeme unaopatikana kwa wateja wa Jimbo la Kigamboni unatoka sub-station ya Ilala. Umeme huu pia husambazwa kwa maeneo ya Temeke, Mbagala na Mkuranga. Kutokana na ongezeko kubwa la mahitaji pamoja na uchakavu wa miundombinu, kumekuwa na ukatikaji wa umeme mara kwa mara.

Tanesco walinieleza kuwa hatua ambazo wanachukua kuondoa tatizo hili ni pamoja na maboresho ya miundombinu, kusafisha njia unaopita umeme huo kwa kukata miti na matawi na kujenga sub-station mpya maeneo ya Mbagala. Kukamilika kwa sub-station ya Mbagala utapunguza utegemezi uliopo sasa kwa sub-station ya Ilala. Kazi ya ujenzi wa sub-station mpya unatarajia kukamilika mwezi Disemba mwaka huu.

2. UMEME MDOGO KWA BAADHI YA MAENEO (LOW VOLTAGE)

Kuna baadhi ya maeneo kama vile Kijichi na Magogoni kumekuwa na tatizo la umeme mdogo. Tanesco walinitaarifu kuwa kuna mpango wa kufanya “voltage improvement” kwa kufanya “phase addition” na kuongeza transfoma nyingine mbili maeneo ya Magogoni. Transfoma zipo na ninatarajia kazi hii itaanza hivi karibuni. Kwa upande wa Kijichi, pamoja na “voltage improvement” bado kutakuwa na tatizo. Suluhu ya kudumu itakuwa kukamilika kwa sub-station ya Mbagala.

Tulikubaliana kuwa kazi hii iwe imekamilika ndani ya miezi mitatu ijayo.

3. UMEME KWA WATEJA WAPYA

Nimekuwa nikipokea malalamiko mengi toka kwa wananchi wengi ambao wamekuwa wakisubiri muda mrefu kupata huduma ya umeme. Malalamiko yamekuwa yakitoka Kibada, Gezaulole, Toangoma, Saku, Rufu na Kiponza.

Uongozi wa Tanesco ulinihakikishia kuwa maandalizi yamekamilika kwa ajili ya usambazaji wa umeme kwenye maeneo ya Kibada (blocks 14,15,16,17,18,19,20).  Waliahidi kukamilisha kazi hii ifikapo mwezi Septemba 2014.

Niliwataka ndani ya wiki tatu (3) kunipa mikakati yao ya kuwapatia umeme wananchi walioomba toka maeneo ya Gezaulole, Mbwamaji, Kizani, Mwera, Kibada(blocks zilizobaki), Ponde, Goroka Kalakala, Masaki na  Malela. Uongozi wa Tanesco uliahidi kufanya hivyo kwani miradi hii imeshatengewa Bajeti zake. Pia, Tanesco haina uhaba wa vifaa vya kuunganisha umeme kwa sasa.

4. MIRADI MIPYA YA UMEME JIMBO LA KIGAMBONI 

Uongozi wa Tanesco ulinitaarifu kuwa maombi yangu ya kutaka Kata za Kimbiji na Pemba Mnazi kuingizwa kwenye mradi wa Umeme Vijijini (REA) yamekubaliwa na sasa kata hizi zitaanza kupata huduma ya umeme.

Kama nilivyoeleza hapo juu, umeme wa sasa kwa Jimbo la Kigamboni hutoka Ilala, ujenzi wa Sub-Station ya Mbagala unaendelea na unatarajia kukamilika mwezi Disemba, 2014. Kukamilika kwa kituo kutafanya baadhi ya maeneo ya Jimbo la Kigamboni kujitegemea kwa huduma ya umeme na pia kuondokana kukatika katika mara kwa mara kwa umeme kama ilivyo sasa.

Vile vile Tanesco ipo kwenye mchakato wa kutafuta eneo katika Tarafa ya Kigamboni kwa ajili ya ujenzi wa sub-station mpya. Katika mwaka huu wa fedha hakuna fedha iliyotengwa kwa mradi huu. Lengo ni kuingiza ujenzi wa sub-station kwenye bajeti ijayo.

Aidha, niliwataka uongozi wa Tanesco kufanya maandalizi ya awali kujua gharama za kufikisha umeme katika maeneo ya Mwasonga, kata ya Kisarawe II ili makisio haya yaingizwe bajeti ya mwakani.Tulikubaliana zoezi hili kufanyika ndani ya miezi mitatu.

5. HITIMISHO 

Shirika la Tanesco halina uhaba wa vifaa kwa sasa. Niliwataka Tanesco Kigamboni kuandaa mpango kazi wa usambazaji wa huduma ya umeme kwa wateja wapya  ambayo itanisaidia kufuatilia utendaji kazi wao; kuboresha mawasiliano na mahusiano na wateja pindi umeme unapokatika au pale wateja wanapofika kuuliza kuhusu hatma ya maombi yao. Kwa vile, Tanesco ina uhaba wa vikosi vya kuunganisha umeme kwa wananchi, niliwashauri waangalie uwezekano wa kutumia wakandarasi binafsi (outsourcing) baadhi ya kazi hizi.

Kwa wananchi wa Kibada, Toangoma na Gezaulole kwa maeneo mliyoniletea orodha zenu, ndani ya siku 21 nitawapatia majibu ya lini maeneo yanatarajiwa kufikiwa. Aidha, nashauri maeneo husika kuunda kamati ambazo zinashirikiana nami katika ufuatiliaji.

Nawasilisha

Dkt Faustine Ndugulile (MB)

Mbunge Kigamboni

Friday, June 20, 2014

UINGEREZA YAPIGISHWA KWATA NA URUGUAY

Mshambuliaji wa timu ya Liverpool Luis Suarez jana aliongoza maangamizi ya kwa timu ya Uingereza dhidi ya timu ya taia lake la Uruguay.
Suarez alikua muiba mchungu kwa Uingereza baada ya kufunga mabao yote mawili na hivyo kuizamisha kwa mabao 2-1.

Suarez akishangilia bao lake la kwanza 
Suarez akifunga bao la pili 
Luis Suarez akishangilia bao la pili na wenzake 
Luis Suarez akiwasikiliza mashabiki kwa furaha 

Thursday, June 19, 2014

IVORY COAST YABAMIZWA NA COLOMBIA

Timu ya taifa ya Ivory Coast leo imefungwa mabao 2-1 na timu ya Colombia katika mashindano ya kombe la dunia yanayoendelea nchini Brazil.

Yaya toure wa Ivory Coast akifanya yake 
 
 




  Gervinho na Tiote wakipongezana

Yaya Toure akisikitika baada ya mchezo kumalizika 
Rodriguez wa Colombia akishangilia na wenzake