Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Tuesday, January 24, 2017

WARAKA WA MH. MBUNGE DKT. FAUSTINE NDUNGULILE KWA WAKAZI WA KIGAMBONI

*TAARIFA KUHUSU BARABARA TOKA DARAJA LA NYERERE NA TOZO ZA DARAJA*
Kwa muda mrefu nimekuwa nikipokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na huduma isiyoridhisha kwenye Daraja la Nyerere linalounganisha Kigamboni na Kurasini.
Malalamiko ya wananchi yako kwenye maeneo makuu matatu:
1. Kutumika kwa madirisha machache ya kukatia tiketi. Daraja la Nyerere lina madirisha 14 ( Saba wakati wa kuingia na Saba wakati wa kutokea). Madirisha yanayotumika ni machache na hivyo kusababisha foleni isiyo na msingi.


2. Tozo za Daraja la Nyerere zipo juu sana hususan kwa magari ya abiria. Hali hii imepelekea Kigamboni kukosa ruti ndefu za kuelekea maeneo mengine ya Jiji la Dar Es Salaam. Gari la abiria linatozwa kati ya Tsh 5000-7000 kwa kila safari ambayo ni gharama kubwa sana kwa kutwa.
3. Kutokamilika kwa kipande kilichobaki toka Darajani hadi kwa Msomali.

Kama Mbunge wa Kigamboni nimekuwa nikifuatilia suala hili kwa karibu sana bila ya mafanikio. Tukumbuke kuwa Daraja la Nyerere lilizinduliwa tarehe 19.04.2016 na sasa ni zaidi ya miezi 9 hamna kinachoendelea na wahusika hawatoi majibu yanayotosheleza.

*HATUA NILIZOCHUKUA HADI HIVI SASA*
1. Mnamo tarehe 15.06.2016 nilimwandikia barua Waziri wa Ujenzi Mhe. Makame Mbarawa (Mb) kuhusiana na hoja hizi. Pamoja na kufuatilia zaidi ya mara kumi kwa simu, maongezi ya ana kwa ana na meseji, barua yangu haijajibiwa hadi hivi sasa (Angalia kiambatanisho).

2. Vile vile nilikutana na Mkurugenzi wa NSSF Prog Godius Kahyarara tarehe 3.10.2016 kuhusu hoja tajwa hapo juu. Aliahidi kuchukua hatua za haraka lakini hadi hivi sasa hakuna kilicofanyika.

3. Kwa kuwa usimamizi wa Daraja la Nyerere upo chini ya NSSF na kipande kilichobaki kitajengwa na NSSF, niliomba kukutana na Waziri anayesimamia taasisi hii. Nilikutana na Mhe. Waziri Jenista Mhagama (Mb) tarehe 3.12.2016 ofisini kwake. Pamoja na maelezo ya mdomo, nilimkabidhi barua ya malalamiko (Angalia kiambatanisho). Mheshimiwa Waziri aliahidi kuchukua hatua za haraka.
Tarehe 13.12.2016 nilipata nakala ya barua aliyoandika Mhe. Waziri Mhagama kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF ili kupata maelezo na ufumbuzi wa hoja nilizotoa. Pamoja na kukumbushia Mhe. Waziri Mhagama hajanipatia majibu ya hoja zangu.


Aidha, maelezo niliyopata toka kwa Mkurugenzi wa NSSF wakati Waziri Mkuu anatembelea Kigamboni tarehe 04.01.2017 ni kwamba fedha zinazohitajika kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kipande kilichobaki ni Tsh 24 Bilioni na alinihakikishia kuwa *FEDHA HIZO ZIPO.* *Michoro (design) ya barabara hiyo IMESHAKAMILIKA.* *Mkandarasi kwa ajili ya kazi hiyo YUPO.*

*Pamoja na NSSF kuwa na fedha ya ujenzi wa barabara hiyo, mkandarasi aliye tayari na michoro iliyokamilika, kumekuwa na kigugumizi ya lini kazi hii itaanza.*
Inasikitisha pia kuona Mawaziri hawajibu barua pamoja na kukumbushwa mara kwa mara.
Kinachoendelea sasa hakuna lugha nyingine ya kuielezea zaidi ya UZEMBE na KUTOWAJIBIKA.
Naleta taarifa hii kwenu wakazi wa Kigamboni ili nanyi mjue kinachoendelea. Ninakusudia kuyapeleka malalamiko yenu kwa mamlaka ya juu zaidi, baada ya mamlaka tajwa hapo juu kushindwa kupata ufumbuzi.

Dkt Faustine Ndugulile Mb
Mbunge
24.01.2017

Tuesday, January 17, 2017

MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA PILI 2016/ 2017 YATOKA


Tayari Serikali kupitia Baraza la mitiani NECTA imetangaza Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2015  324,068 sawa na 89% kati ya wanafunzi 363,666 waliofanya mtihani wamefaulu kuendelea na kidato cha tatu kwa mwaka 2016.
Matokeo yote unaweza kuyatazama hapa.


Pia unaweza kupata matokeo kwa kutuma SMS kwenda 15311. Kwa kufuata maelekezo yafuatayo..






































Send SMS to 15311
How to send SMS
  1. To get results: Write:
    matokeo*centre number*candidate number*exam type*exam year
    Example :
    matokeo*S1665*0041*k4*2014
    matokeo*M0110*0003*qt*2014
  2. To get rank: Write: rank*centre number*exam type*exam year Example : rank* S0101*k4*2014
Cost per SMS is Tshs 200/=
This service is only available for Tigo, Vodacom and Zantel subscribers.