Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Thursday, February 9, 2017

BREAKING NEWS....... MAJIBU SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA

GWAJIMA NAE AONGEA NA WAANDISHI WA HABARI...
Mchungaji wa kanisa la Saa ya Ufufuo  Bw. Josephat Gwajima leo hii ameongea na waandishi wa habari akiwa na jopo l a maaskofu wake wasaidizi. Dhumuni la kuongea na waandishi hao ilikuwa ni kutoa ufafanuzi wa kuhusishwa kwake katika sakata linaloendelea nchini la kupambana na uingizaji na utumiaji wa madawa ya kulevya.




Akijibu maswali ya waandishi wa habari , Mchungaji gwajima alieleza kuwa anakubali kazi nzuri inayofanywa na Mh. Mkuu wa Mkoa lakini akisisitiza kuwa mkuu huyo hana uwezo wa kutawaLA na hivyo atatuma maombi kwa Mh. Rais ili apangiwe kazi nyingine.

Pia alisisitiza kuwa ataenda katika kituo cha kati cha polisi kuitikia wito siku ya leo na sio kesho kama alivyotakiwa na amesema yupo tayari kukaa ndani kwa miaka hata 40 kwa kuwa kama atabainika ana makosa.

Alipoulizwa kuhusu upatikanaji wa mali lukuki alizonazo, alieleza kuwa mali hizo zinatokana na jasho lake kwa kuwa amekuwa mhadhiri wa kimataifa wa dini huku akipata kiasi cha dola za kimarekani 1000 kwa kila kipindi. Pia alieleza kuwa kanisa lake lina kampuni ambayo huingiza pesa nyingi na yeye akiwa kama mkurugenzi wa kampuni hiyo. Alipoulizwa kuwa haoni sababu ya kuhusishwa na madawa ya kulevya imetokana na urafiki wake wa karibu na Waziri mkuu mstaafu aliyekuwa mgombea wa UKAWA, alijibu kuwa mambo ya uchaguzi yalishapita na sasa yeye anamuunga mkono Mh. Rais Magufuli.

Mwisho alisema kuwa wito wake aliusikia Redioni  lakini kwa unyenyekevu leo ataenda kuonana na kamanda wa polisi Siro katika kituo cha Polisi kati.

SAKATA LA VITA DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA...MANJI AITIKIA WITO LEO POLISI

Mfanyabiashara mashuhuri nchini Yusuph Manji leo aliitikia wito wa mkuu wa Mkoa Mh. Makonda wa kuripoti katika kituo cha kati cha Polisi kwa ajili ya mahojiano kuhusu vita dhidi ya madawa ya kulevya. Hata hivyo Manji ambaye alitakiwa afike kituoni hapo siku ya Ijumaa amefika leo kituoni hapo huku sababu za kuwahi kwake zikiwa hazijulikani.

Picha na ripota wetu.

      Mashuhuda wakishuhudia




 Akiwasili....




Akiongea na baadhi ya Wadau

VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA RC MAKONDA AWATAJA MBOWE, MANJI, GWAJIMA, IDD AZZAN...

Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Dsm,ndugu Paul Makonda ameongea na waandishi wa habari kuhusu muendelezo wa vita ya madawa ya kulevya ktk jiji la Dsm.



Mh. Paul Makonda amsema anataka wauzaji wa dawa za kulevya wajulikane hadharani na hakuna sababu ya kuficha. Pia ameasema vita vya dawa za kulevya vilianza muda mrefu kwa kufutilia hali ilivyo mitaani. “Kuna watu nilitaka nikutane nao polisi, kuna tofauti kati ya kukamatwa na kuitwa, unapoitwa unapewa nafasi ya kusikilizwa”Alisema-RC Makonda. Aliendelea kwa kusisitiza


“Kampeni hii dawa ya dawa za kulevya si ya kufanyika kimyakimya tunataka hata watoto wadogo wajue dawa hizi ni hatari kwa afya”-RC Makonda

“Asante kwa watu kama TID, nawapongeza kwa kukiri na kusema kuwa wanatambua namna walivyoingia na kuomba serikali kuwasaidia”-RC Makonda

“Tumemaliza awamu ya kwanza vita ya dawa za kulevya, sasa hii ni awamu ya pili ambayo itakuwa si nyepesi itakuwa na mawimbi mengi”-Makonda

“Awamu ya 2 ya vita ya dawa za kulevya tunaianza leo na tunaianza tukiwa tumekamilika, nimekuwa kwenye operesheni usiku na mchana”- Makonda