Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Thursday, February 9, 2017

VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA RC MAKONDA AWATAJA MBOWE, MANJI, GWAJIMA, IDD AZZAN...

Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Dsm,ndugu Paul Makonda ameongea na waandishi wa habari kuhusu muendelezo wa vita ya madawa ya kulevya ktk jiji la Dsm.



Mh. Paul Makonda amsema anataka wauzaji wa dawa za kulevya wajulikane hadharani na hakuna sababu ya kuficha. Pia ameasema vita vya dawa za kulevya vilianza muda mrefu kwa kufutilia hali ilivyo mitaani. “Kuna watu nilitaka nikutane nao polisi, kuna tofauti kati ya kukamatwa na kuitwa, unapoitwa unapewa nafasi ya kusikilizwa”Alisema-RC Makonda. Aliendelea kwa kusisitiza


“Kampeni hii dawa ya dawa za kulevya si ya kufanyika kimyakimya tunataka hata watoto wadogo wajue dawa hizi ni hatari kwa afya”-RC Makonda

“Asante kwa watu kama TID, nawapongeza kwa kukiri na kusema kuwa wanatambua namna walivyoingia na kuomba serikali kuwasaidia”-RC Makonda

“Tumemaliza awamu ya kwanza vita ya dawa za kulevya, sasa hii ni awamu ya pili ambayo itakuwa si nyepesi itakuwa na mawimbi mengi”-Makonda

“Awamu ya 2 ya vita ya dawa za kulevya tunaianza leo na tunaianza tukiwa tumekamilika, nimekuwa kwenye operesheni usiku na mchana”- Makonda

No comments:

Post a Comment