Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Thursday, February 9, 2017

BREAKING NEWS....... MAJIBU SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA

GWAJIMA NAE AONGEA NA WAANDISHI WA HABARI...
Mchungaji wa kanisa la Saa ya Ufufuo  Bw. Josephat Gwajima leo hii ameongea na waandishi wa habari akiwa na jopo l a maaskofu wake wasaidizi. Dhumuni la kuongea na waandishi hao ilikuwa ni kutoa ufafanuzi wa kuhusishwa kwake katika sakata linaloendelea nchini la kupambana na uingizaji na utumiaji wa madawa ya kulevya.




Akijibu maswali ya waandishi wa habari , Mchungaji gwajima alieleza kuwa anakubali kazi nzuri inayofanywa na Mh. Mkuu wa Mkoa lakini akisisitiza kuwa mkuu huyo hana uwezo wa kutawaLA na hivyo atatuma maombi kwa Mh. Rais ili apangiwe kazi nyingine.

Pia alisisitiza kuwa ataenda katika kituo cha kati cha polisi kuitikia wito siku ya leo na sio kesho kama alivyotakiwa na amesema yupo tayari kukaa ndani kwa miaka hata 40 kwa kuwa kama atabainika ana makosa.

Alipoulizwa kuhusu upatikanaji wa mali lukuki alizonazo, alieleza kuwa mali hizo zinatokana na jasho lake kwa kuwa amekuwa mhadhiri wa kimataifa wa dini huku akipata kiasi cha dola za kimarekani 1000 kwa kila kipindi. Pia alieleza kuwa kanisa lake lina kampuni ambayo huingiza pesa nyingi na yeye akiwa kama mkurugenzi wa kampuni hiyo. Alipoulizwa kuwa haoni sababu ya kuhusishwa na madawa ya kulevya imetokana na urafiki wake wa karibu na Waziri mkuu mstaafu aliyekuwa mgombea wa UKAWA, alijibu kuwa mambo ya uchaguzi yalishapita na sasa yeye anamuunga mkono Mh. Rais Magufuli.

Mwisho alisema kuwa wito wake aliusikia Redioni  lakini kwa unyenyekevu leo ataenda kuonana na kamanda wa polisi Siro katika kituo cha Polisi kati.

No comments:

Post a Comment