Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Sunday, December 7, 2014

MDAU WENU NILIPOTEMBELEA MOJA YA MAAJABU 7 YA DUNIA KASRI YA TAJ MAHAL NCHINI INDIA

Mdau wenu nilipokuwa dhiarani nchini India, moja ya maeneo niliyofanikiwa kuyatembelea ilikuwa ni pamoja na makumbusho ya Kasir ya mfalme wa zamani aliyewahi kutawala nchini India. Kivutio kikubwa katika kasri hiyo kubwa iliyosheheni vito vya thamani ni makaburi mawili makubwa ya mke wa tatu wa mfalme huyo pamoja na kaburi la mwanae. Inasemekana mfalme huyo aliyejaliwa kuwa na wake watatu alimpenda sana mke wake wa tatu na hata kuamua kumjengea kasri hiyo ili atakapokufa mwili wake uhifadhiwe humo. Kasri hiyo iliyojengwa na watumishi wapatao 1400 ilikamilika katika kipindi cha miaka 4 na kila mfanyakazi aliyehusika katika ujenzi huo baada ya kumalizika kwa ujenzi mfalme aliamuru akatwe kiganja cha mkono wa kulia kusudi wasiweze kujenga mfano wa kasri hiyo popote hapa duniani. Kasri hii kubwa nchini India ni moja kati ya maajabu saba ya Dunia.
Sanamu ya mfano wa Kasri ya Taj Mahal
Raia mbalimbali wa Kigeni wakiangalia moja ya maajab ya dunia ya Taj Mahal nchin India
 
Mdau nikiwa mbele ya Kasri ya Taj Mahal 
Kila anaefika mahali hapa anapenda kupiga picha ya muonekano huu
 

No comments:

Post a Comment