Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Thursday, January 31, 2013

MWANAMKE AWEKA SUMU UKENI ILI KUMUUA MUMEWE


Ilisemwa ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni. Huko nchini Brazil mwanamke mmoja ambaye alikuwa amemchoka mumewe na hivyo kutaka kuachana naye aliamua kufanya jambo moja baya sana ambalo si kwamba lingemdhuru mumewe tu, bali pia lingemdhuru hata yeye mwenyewe na pengine hata kupoteza maisha wote wawili.

Mwamamke huyo badala ya kuomba talaka au hata kujiondoa katika ndoa hiyo ambayo kwake aliiona haina maana aliamua kumuwekea sumu mumewe aliyekuwa na umri wa miaka 43. 

Lakini hakuweka sumu hiyo katika chakula, na badala yake akaweka sumu hiyo katika uke wake, na kisha kumshawishi mumewe kufanya naye mapenzi lakini alimuomba aende chumvini, (Kulamba uke) (Oral Sex) mahali ambapo ndipo alipoweka sumu hiyo. 

Mumewe bila kujua alizama chumvini, lakini alishtushwa na harufu kali ya kemikali asiyoijua ikitokea kunako uke wa mkewe na hapo ndipo mchezo mzima uliposhtukiwa.

Kuona hivyo mumewe alimshauri ampeleke huyo mkewe hospitali akijua amepata tatizo katika uke wake. Mkewe alikubali na baada ya kumfikisha katika Hospitali iliyoko katika mji huo wa San Jose do Rito Preto, alifanyiwa vipimo na madakatari. 

Madakatari hao waligundua kwamba mwanamke huyo aliweka sumu kwenye uke wake ili kumuua mumewe na yeye pia. Mwanamke huyo alikiri kufanya jambo hilo kwa makusudi kabisa. Alipatiwa matibabu na kisha kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Hata hivyo mumewe amedai atamshitaki huyo mkewe kwa jaribio la kutaka kumuua.

Source: JF

No comments:

Post a Comment