Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Friday, May 5, 2017

HIMID MAO AANZA KUFANYA MAJARIBIO DENMERK

NAHODHA Msaidizi wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Himid Mao ‘Ninja’, anaendelea na majaribio yake kwenye kikosi cha Randers inayoshiriki Ligi Kuu nchini Denmark.

Himid tayari ameshafanya mazoezi mara mbili juzi na jana akiwa na kikosi cha wachezaji wa akiba wa timu hiyo, ambapo leo Jumatano alipewa mapumziko kabla ya kesho Ijumaa kuanza rasmi kujifua na kikosi cha kwanza cha Randers.

Kwa mujibu wa mtandao wa klabu hiyo, umeeleza kuwa kiungo huyo nyota mkabaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, 24, yuko tayari kwa mara ya kwanza kucheza soka la kulipwa na kulipa kisogo soka la nyumbani kwa kuhakikisha anapata mkataba wa kusajiliwa na Randers.

#StayStrongHimidMao23 #GoodLuck

No comments:

Post a Comment