Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Wednesday, August 15, 2012

WALIOFANYA VIZURI KIDATO CHA SITA WAPONGEZWA


WANAFUNZI 20 waliofanya vizuri katika mitihani yao ya kumaliza kidato cha sita mwaka huu wamepongezwa na Bunge pamoja na kukabidhiwa zawadi mbalimbali, ikiwamo fedha taslimu sh 200,000 kila mmoja.
Hafla ya kuwapongeza wanafunzi hao kutoka shule nane za serikali na mbili za binafsi ilifanyika bungeni jana baada ya Bunge kutengua kanuni na kuruhusu wanafunzi hao kuingia ukumbini.
Mbali na fedha taslimu, wanafunzi hao walipewa zawadi za kompyuta ndogo (Laptop) na cheti ambavyo walikabidhiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Pia kila shule iliyotoa mwanafunzi au wanafunzi bora imezawadiwa sh milioni moja.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema jana kuwa hafla hiyo inafanyika ili kuwaenzi na kuwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri.

No comments:

Post a Comment