Sendoff ya Bi. Safii Ramadhani imefanyika usiku wa leo katika ukumbi wa Msasani Club na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali. Bi Safii anatarajia kufunga ndoa na Bw. Yusuph Mdoe Mwasala siku Ijumaa tarehe 21 na Sherehe siku inayofuta ya tarehe 22.
Wednesday, June 19, 2013
Monday, June 17, 2013
MATUMAINI YA TANZANIA KWENDA WORLD CUP BRAZIL 2014 YAYEYUKA
Ndoto za Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars" kufuzu mzunguko wa pili wa kushiriki fainali za Kombe la Dunia 2014 huko Brazil zilifutika jana kwenye Uwanja wa taifa jijini Dar-es-Salaam baada ya kukubali lkipigo cha mabao 2-4 mbele ya Tembo wa Ivory Coast.
Katika mechi ya hiyo Stars walipata bao la kwanza katika dakika ya kwanza ya mchezo lililofungwa na Amri Kiemba baada ya beki wa Ivory Coast kujichanganya. Bao la pili la kusawazisha lilifungwa na straika Thomas Ulimwengu kabla ya Ivory Coast kufunga bao yake kupitia kwa Yahya Toure aliyefunga mawili, Lacina Traore na Willfred Bony waliofunga goli moja kila mmoja. Tanzania licha ya kufungwa ilionyesha mchezo mzuri uliowabana Ivory Coast katika kipindi chote cha mchezo.
Umati wa wapenda kandanda ulioudhulia pambano.
BOMU LAUA WAWILI ARUSHA KATIKA MKUTANO WA CHADEMA
Mlipuko wa Bomu la kurushwa ulitokea Arusha na kusababisha vifo vya watu wawili na kujeluhi wengine 70 wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Udiwani wa Chama cha Chadema uliofanyika katika Uwanja wa Soweto Kata ya Kaloleni mjini Arusha. Mkutano huo ulikuwa ukiendeshwa na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha mjini Mh. Godbless Lema ambao wote wawili walinusurika. Serikali na uongozi mzima wa blog hii unalaani vikali vitendo hivi vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Mungu ibariki Tanzania.
Mmoja kati ya watoto walioathirika na mlipuko
Sunday, June 16, 2013
MDAU YUSUPH MDOE AANZA WIKI YA HARUSI
Mdau Yusuph Mdoe ameanza pilika za wiki ya harusi kwa kufanyiwa Beg Party katika ukumbi wa vijana kinondoni huku akisindikizwa na marafiki zake ambapo alizawadiwa zawadi kemkem.
Siku ya Jumatano tarehe 19 ndio itakuwa send off ya mtarajiwa wake kipenzi katika ukumbi wa Msasani Beach.
Keki mfano wa Uwanja wa Emirate ikiwa na nembo ya Arsenal.
Bwana harusi mtarajiwa na mpambe wakiselebuka.
Mduara kuduwarika!
Yusuph na marafiki
Marafiki wa Bwana harusi mtarajiwa wakiinua vitambaa vyeupe.
Friday, May 24, 2013
KONGAMANO LA MAAFISA UNUNUZI NA UGAVI LAANZA MOROGORO
Kongamano la pili la maafisa Ununuzi na Ugavi Serikalini limeanza leo mjini Morogoro katika ukumbi wa Hoteli ya Nashera.
Kongamano hilo lililoandaliwa na Idara Sera ya Ununuzi wa Umma chini ya Wizara ya Fedha likiwa na kauli mbiu "Ununuzi Makini kwa Maendeleo ya Taifa" linatazamiwa kuwa la siku mbili kuanzia tarehe 24-25 Mei 2013.
Wajumbe wa Mkutano
Wajumbe wa Sekretarieti
Wajumbe wa Sekretarieti.
Sunday, May 12, 2013
MABALOZI WA UMOJA WA ULAYA WASHEHEREKEA SIKU YAO KWA KUCHEZA MECHI NA WIZARA YA FEDHA
Mabalozi wa nchi za Umoja wa Ulaya EU jana walisheherekea siku yao kwa kufanya bonanza la mpira wa miguu katika uwanja wa Karume kwa kupambana na timu ya Wizara ya Fedha (Hazina Sports).
Matokeo katika mchezo huo ni kwamba Mabalozi wa EU waliondoka uwanjani kifua mbele kwa ushindi wa mabao 5-2 dhidi Wizara ya fedha
Zawadi ya Ngao kama ishara ya Ushirikiano
Timu ya Wizara ya Fedha
Timu ya Mabarozi wa Ulaya
Timu zote mbili kwa pamoja baada ya mchezo.
Sunday, May 5, 2013
BOMU LALIPUKA NA KUJERUHI KANISANI ARUSHA
Bomu linalosemekana ni la kurusha limelipuka na kujeruhi watu kadhaa kanisani mkoani Arusha. Vyanzo vya habari vinadai bomu hilo lililipuka wakati wa sherehe za ufunguzi wa kanisa.
Baadhi ya majeruhi wakiugulia maumivu makali mara baada ya mlipuko
Friday, May 3, 2013
SODOMAAAA!!! KANGA MOJA WAJA NA STAILI YA KUJIMWAGIA POMBE!
Kikundi cha kucheza michezo ya wakubwa maarufu jijini kama kanga Moja laki si Pesa wamekuja na staili chafu ya kumwagia pombe makalio wakati wa kucheza! Naomba radhi kwa picha hizi ila ndio ukweli wenyewe.
Thursday, May 2, 2013
BONANZA LA MEI MOSI LEADERS CLUB LATIA FORA
Bonanza la Mei Mosi lililoandaliwa na kampuni ya Butterfly Advertising wakishirikiana kipindi cha Sports Extra kinachorushwa na Clouds FM chini ya mtangazaji Shafii Dauda lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club siku ya Mei Mosi lilifana kwa kupendeza.
Tamasha hilo lilizishirikisha timu za mpira wa miguu kutoka makampuni mbali mbali yakiwemo Benk ya CRDB, NMB,Vodacom, FastJet, NSSF, Tanesco, Umoja water, NHC, Clouds FM na DHL.
Tamasha hilo lilizishirikisha timu za mpira wa miguu kutoka makampuni mbali mbali yakiwemo Benk ya CRDB, NMB,Vodacom, FastJet, NSSF, Tanesco, Umoja water, NHC, Clouds FM na DHL.
SIKUKUU YA MEI MOSI YAFANA
Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi ilisheherekewa kwa namna yake ulimwenguni huku ha kwetu tanzania ikipambwa na maandamano ya wafanyakazi katka viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar-es-Salaam. Katika sherehe za mwaka huu, rais wa Jamhuri ya Tanzania Dr. Mrisho Jakaya Kikwetealihaidi serikali kupunguza kodi ya mshahara kwa wafanyakazi. Habari zaidi katika picha.
Wednesday, May 1, 2013
BAHATI YAITOA MADRID UEFA
Timu ya Real Madrid ya Hispania usiku wa leo wamelala vibaya baada ya kujikuta wanaondoshwa katika nusu fainali ya kombe la UEFA na klab ya Dortmund ya Ujerumani kwa idada ya mabao 4-2 baada ya kucheza mchezo wa marudiano.
Subscribe to:
Posts (Atom)