Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Tuesday, June 30, 2015

WALIMU WANYANYASWA KISHIRIKINA BUNDA

MBUNGE wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola amelazimika kukatisha vikao vya Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma kwenda jimboni kwake, kijiji cha Nambaza, kata na tarafa ya Nansimo, wilaya ya Bunda mkoani Mara kushughulikia adha wanayoipata walimu wa shule ya msingi kijijini hapo wanaofanyiwa vitendo vya kishirikina, kudhalilishwa na kuteswa kishirikina na kulazimika kuomba uhamisho wakafundishe shule nyingine maeneo ya mbali na jimbo hilo.

Walimu wa shule hiyo ya msingi Nambaza wanadai usiku wakiwa wamelala wanaingiliwa na wachawi ambao wamekuwa wakiwanyoa nywele sehemu za siri, kuwafanyia vitendo vya ngono, kuwalawiti na kuwaibia mali na fedha kishirikina.

Aidha walimu hao wanadai kwamba, mbali na vitendo hivyo vya kuingiliwa kimwili, kulawitiwa, kunyolewa nywele sehemu za siri, kuibiwa mali na fedha kishirikina, pia wamekuwa wakikuta mikojo, ugali na samaki ukiwa umefunikwa na shuka kitandani, hali ambayo imewafanya washindwe kufundisha na kuomba wahamishwe katika shule hiyo.

Mwalimu Joyce Maugo ambaye ni mkongwe kidogo katika shule hiyo, kwa masikitiko huku akibubujikwa na machozi alisema, walimu wa shule hiyo wako hatarini kwa vitendo vya kishirikina wanavyofanyiwa, alisema mmoja wa walimu wenzake, msichana mdogo na mdogo kimaumbile aliingiliwa kimwili kishirikina mpaka kazimia.

Alisema, asubuhi alipoitwa kwenda kushuhudia yaliyomkuta mwalimu huyo mwenzake,  alikuta mambo ya aibu amefanyiwa mwalimu huyo, alikuwa hawezi kutembea, sehemu zake za siri zikiwa zimeharibiwa vibaya, kitanda kikiwa kimevurugwa hovyo hovyo, kikiwa na kinyesi, damu na mikojo kibao!

Bi. Joyce alisema mwalimu wa kiume Pasco Mayamba akiwa amefunga milango na madilisha ya chumba chake, asubuhi alipoamka alikuta madirisha na milango iko wazi, kitanda kimejaa mkojo, kitandani kwake ndani ya shuka alilojifunika kukiwa na bonge la ugali, kipande cha mnofu wa sangara na mchuzi mwingi.

Alisema, wakati fulani wakila chakula usiku, ghafla chakula kinabadilika, kama ulikuwa wali na nyama unakuwa ugali na dagaa au mboga za majani hali ambayo alisema ni ya mateso, adha na manyanyaso makubwa wanayoyapata nakuomba wahurumiwe, kama kuna makosa wamewafanyia wawaambie wawaombe msamaha ili wasiendelee kuwatesa na kuwanyima raha na amani kimaisha.

Mwalimu Lucy alisema, mbali na adha hizo watu hao wanawaibia fedha, vitambulisho, kadi za benki na mali nyingine, lakini pia wakati mwingine wanakuta mkojo na kinyesi katika madebe ya unga na chungu cha mboga vitendo ambavyo vinawanyima morari ya kazi na ari ya kuendelea kufundisha shule hiyo.

Kwa sasa mwalimu Lucy alisema watu hao wanahisaidia haja kubwa madarasani na kuwapa kibarua walimu na wanafunzi kuzoa kinyesi madarasani karibia kila siku na kuwasihi viongozi na wanakijiji wa kijiji hicho waliowema kuchukuwa hatua dhidi ya madhira hayo kwa walimu.

Akizungumza na majira jana akiwa mjini Bunda, mbunge Kangi alisema vitendo vya kishirikina wanavyofanyiwa walimu hao ambao ni wageni,  waliopelekwa shuleni hapo hivi karibu siyo vya kufumbiwa macho, ni vya kukemewa vikali na wahusika wakibainika wachukuliwe hatua kali kwani, mbali na madhara wanayoyapata walimu hao kwa kuingiliwa kimwili bila ridhaa yao na watu wasiowajua wala kuwaona,  pia vinawadhalilisha na vinalenga kudidimiza maendeleo ya elimu katika jimbo lake.

Kangi alisema,  amelazimika kwenda kijijini Nambaza kulishughulikia tatizo hilo ambapo leo Jumatatu, Juni 29, 2015 atafanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji hicho ili kutafuta ufumbuzi na dawa ya tatizo hilo ili likomeshwe na lisitokee tena.

Wananchi wa kijiji hicho katika mkutano wao wa hadhara walioufanya hivi karibuni waliwabaini kwa kuwapigia kura baadhi ya wanakijiji hicho kuwa ni wahusika wakuu katika kuwafanyia vitendo hivyo vya kishirikina walimu hao, kiongozi na kinara wa mch ezo huo mchafu akitajwa mmoja wa viongozi kijijini hapo anayeishi eneo jirani na shule hiyo.

Wanakijiji wa kijiji hicho waliazimia washukiwa hao wahame haraka kijijini hapo kabla hawajachukua sheria mkononi wakidai vitendo wanavyo vifanya mbali na kuvunja sheria vitasababisha shule yao ikose walimu wa kuwafundisha watoto wao hali ambayo  inaweza kusababisha kijiji kukosa wasomi na kuwa kijiji cha wahuni na vibaka.

Kuhusu maamuzi ya wanakijiji hao ya kuwataka wakazi wenzao, wanaowatuhumu kwa ushirikina kuhama kijiji, mbunge Kangi alisema, atayaheshimu maamuzi yao na kwamba kabla wananchi hawajafikia hatua ya kuchukua sheria mkononi atawashauri watu hao wahame kijiji hicho haraka.

Mkuu wa wilaya ya Bunda, Joshua Milumbe aliliambia majira kwamba, vitendo hivyo hawezi kuvivumilia, ni vitendo vya udhalilishaji, asivyoweza kuvifumbia macho lazima achukue hatua.

Mkuu wa wilaya Milumbe alisema, atakwenda Nambaza kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho na kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa sheria atachukua hatua kali dhidi ya watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo vya kihuni akisisitiza ataheshimu maamuzi ya wananchi.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bunda Bi. Lucy Msofe alisema,  amesikitishwa sana na vitendo hivyo wanavyofanyiwa walimu hao wenye umri mdogo na wadogo kwa maumbile akidai ni ukatili wa hali ya juu wanaofanyiwa walimu hao.

Bi. Msofe alisema, tayari amelazimika kumuhamisha mwalimu mmoja wa kike ambaye alifika kwake akiwa na hali mbaya kutokana na alivyofanyiwa na watu hao na kuongeza kwamba, endapo hali hiyo itaendelea atalazimika kuwahamisha walimu katika shule hiyo awapeleke katika shule wanayowahitaji,kuwaheshimu na kuwathamini kwani uenda shule ya msingi Nambaza hawahitajiki.

Alisema hayuko tayari kuendelea kushuhudia watoto wa watu wakiendelea kuteseka, kunyanyasika, kudhalilishwa na kufanyiwa unyama kiasi hicho akadai atawahamisha kama vitendo hivyo havitakomeshwa.

Thursday, April 9, 2015

HABARI MVUNJIKO...! AJALI MBAYA YA MABASI YATOKEA LEO

Ajali mbaya imetokea leo kati ya dasi la Ngorika na RATCO na gari ndogo na kusababisha vifo vya watu tisa na wengine wengi kujeruhiwa. Vyanzo vimedai kuwa ajali hiyo ilisababishwa na dereva wa basi la RATCO aliyekuwa akikilipita garo dogo


 
 
 
 
 

Friday, March 6, 2015

LIVE KUTOKA KATIKA MARRIAGE REVIVAL DENNER PATY

Baadhi ni matukio yanayoendelea katika dinner Party ya Marriage Revival kutoka kanisa la Mlima wa moto Mikocheni.
Washiriki wakifuatilia kwa umakini... 

Saturday, February 14, 2015

VIKOSI VYA KIGAIDI VYAJERUI ASKARI POLISI WANNE KATIKA MAPAMBANO TANGA.

Kumekuwa na mapambano yanayoendelea katika mapango ya amboni kati ya askari wa jeshi la polisi na kikundi cha kigaidi kinachosemekana kuweka kambi katika mapango hayo.
Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa katika mapambano hayo ya kivita askari wa nne wamejuruhiwa vibaya. Tutawaletea taarifa kadri zitakavyokuwa zinapatikana. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Askari akiwa katika doria.
 
Askari wakishuka katika helikopta tayari kwa mapmbano. 
 
Kituo cha Habari ITV kikitangaza mapigano hayo. 

HAPPY VALENTINE DAY

Managment ya Njia ya Kanani Blog inapenda kuwatakia wadau wote siku njema ya wapendanao duniani na kusihi tudumishe upendo na amani miongoni mwetu.

Tuesday, February 3, 2015

FAHAMU JINSI UMEME UNAOVUJA (LEAKAGE) UNAVYO KUONGEZEA GHARAMA KATIKA BILI YAKO YA UMEME

HUU NDIYO UFUMBUZI WA BILI KUBWA YA UMEME

Wengi wamekuwa wakilipa bili kubwa za umeme ambazo hata wao wanahisi sio halali ukilinganisha na matumizi yao.
Tatizo la kuvuja kwa umeme limekuwa kubwa sana,bahati mbaya mafundi wengi wamekuwa wakilitatua kwa namna ya kuliongeza badala ya kuliondoa. Tatizo hili limekuwa likitokea sana katika nyumba ambazo zinatumia vifaa vya pin tatu yaani live,neutral and earth mfano fridge,pasi,jiko la umeme, n.k.Vile vile linatokea sana katika nyumba yenye wiring iliyo choka au kwenye nyumba ambayo wire zake zimechubuka.

Kwa kawaida kuna vifaa maalumu vya kutambua uvujaji wa umeme katika nyumba kama vile EARTH LEAKAGE CIRCUIT BREAKER ingawaje nyingi zilizo fungwa majumbani siku hizi ni FEKI hivyo zinashindwa kujizima pale umeme unapo vuja.
Mara nyingi Leakage ya umeme hua inapimwa kwa kuangalia resistance between LIVE wire and EARTH wire na kiutaratibu laizima resistance ya wire hizi mbili izidi 1000000 ohms =1mega ohms Kama endapo itatokea ikwa chini ya hapo moja kwa moja tunaamini kuna gharama za ziada zitakazo ongezeka kutokana na resistance hiyo kushuka chini ya kiwango hicho. Mfano fundi umeme amepima continuity na kukuta resistance between LIVE wire and EARTH wire is 1000 ohms = 1k ohms
Mweye nyumba yenye ukinzani kama huu ataingia gharama ya ziada ambayo inasababishwa na kuvuja kwa umeme. 

HEBU TAZAMA MFANO HUU HAPA CHINI KULINGANA NA RESISTANCE HIYO HAPO JUU ITAONGEZA GHARAMA KIASI GANI KWA MTUMIAJIWA UMEME.
(i) Resistance between LIVE wire and EARTH wire = 1000 ohms
(ii) Tafuta Current (I) Current (I) =V/R
NOTE:-Umeme unaoingizwa majumbani wa single phase ni 220 Voltage.
Hivyo Current(I) =V/R = Current (I) =220/1000=0.22Ampere
(iii) Tafuta power Power (P) =Voltage(V) X Current(I) Hivyo P=VxI P=220 x 0.22= 48.4 watt
P=48.4watt.
NOTE:-Gharama za Unit moja ya tanesco ambayo ni sawa na 1000watt ni 306.52Tsh,hii ni kwa wale wanao tumia zaidi ya Unit 50Kwh.

TAZAMA JEDWALI HILI KWA UFAFANUZI ZAIDI:
Domestic Low Usage Tariff (D1)
This category covers domestic customers who on average have a consumption pattern for 50 kWh. The 50 kwh are subsidized by company are not subjected to service charge. Under the category any unit exceeding 50 kwh is charged a higher rate up to 306.52Tsh. In this tariff category, power is supplied at a low voltage, single phase (230 V).

General usage Tariff (T1)
This segment is applicable for customers who use power for general purposes: including residential, small commercial and light industrial use, public lighting, and billboards. In this category the average consumption is more 306.52Tsh. per meter reading period. Power is given at low voltage single phase (230), as well as three phase (400V).

Low voltage maximum Demand (MD) usage tariff (T2)
Applicable for general use where power is metered at 400V and average consumption is more than 7,500kWh per meter reading period and demand doesn’t exceed 500KVA per meter reading period. High Voltage Maximum Demand (MD) usage tariff (T3).
Applicable for general use where power is metered at 11KV and above.

Tariffs:
Domestic Low Usage (D1)
General Usage (T1)
Low Voltage Max (T2)
High Voltage Max (T3)

NOTE:
All the charges above exclude VAT and EWURA Au tembelea Tanesco Electricity Charges.

Kama tulivyoona 1unit it cost 306.52Tsh if your consumption is more than 50Kwh
Hivyo basi Tukitaka kujua gharama za uvujaji wa umeme kwa resistance hiyo hapo juu (gharama hii ni ya umeme unao vuja bila kujali umetumia umeme au hujatumia) ni kama ifuatavyo:-
Cost = (Consumption watt /1000) x Time x 306.52 Kwh Cost =
(48.4w/1000w) x 720 hrs x 306.52Kwh=10,681.6Tsh
Cost consumption is 10,681.6Tsh.

Hivyo kama resistance between LIVE wire and EARTH wire is 1000 ohms you have fixed added cost of 10,681.6Tsh on your normal consumption cost. Hii inamaanisha kama matumizi yako ya ndani ya halali unayotumia mfano ni ya 52000 itakubidiulipe 62681.6Tsh badala ya 52000.
NOTE:-
The added cost may either decrease or increase due to the either increase or decrease of the resistance respectively between live wire and earth wire
This means the high the resistance between the LIVE wire and the EARTH wire=low added cost and the low resistance between the LIVE wire and the EARTH wire=high added cost
IT SUGGESTED THAT THE RESISTANCE BETWEEN THE LIVE WIRE AND THE EARTH WIRE SHOULD BE MORE THAN 1000000 ohms = 1mega ohms
THIS IS APPLIED THE SAME TO THE RESISTANCE BETWEEN LIVE WIRE AND NEUTRAL WIRE DURING “off state” OF THE CIRCUIT.

Kama unahisi unalipa bili ya umeme zaidi ya matumizi yako hakikisha unawasiliana na fundi umeme aje kukupimia continuity ya wiring yako.
ZINGATIA:-Kitaalamu uvujaji wa umeme unaopelekea kuongezeka kwa bili ya umeme hakutibiwi kwa kubadilisha EARTH ROAD kama wengi wanavyo fanya,utaweza kuondoa tatizo hilo kwa ku-trace eneo linalo vujisha umeme na kuliondoa.
HAKIKISHA FUNDI WAKO ANA KIFAA CHA KUPIMIA CONTINUITY “MEGA” ILI AWEZE KUTAMBUA RESISTANCE BETWEEN THE WIRES ON YOUR CIRCUIT.
Any obtained resistance can help to determine the added cost by above formula.
PENDELEA KUKAGUA WIRING YAKO KILA BAADA YA MIEZI SITA KWA USALAMA WA UCHUMI WAKO, MALIZAKO NA UHAI WAKO.



IBRAHIM ABDALLAH MAKBEL
C.E.O FAABI ELECTRICAL AND SECURITY SYSTEM

MAWASILIANO:
+255787577755
+255767577755
+255717577755
+255777077755
FAABI TEAM TUPO KWA AJILI YENU NA MALI ZENU.
Email: faabielectrical@gmail.com

 

Monday, January 5, 2015

BREAKING NEWS!! MABASI MATANO YAPATA AJALI YAKITOKEA KILIMANJARO

Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba kuna mabasi matano yamegongana njia ya kwenda Arusha toka Dar-es-Salaam asubuhi ya leo. Habari za kuaminika zinasema moja ya mabasi hayo ni Kilimanjaro Express na hadi sasa bado haijajulikana idadi ya majeruhi wala waliopotenza maisha ni wangapi. Punde itawajia habari kamili.

 
 
 
 

Friday, January 2, 2015

BREAKING NEWS!!! PANYA ROAD WAITIKISA DAR USIKU HUU

TAHARUKI YA 'PANYA ROAD': Kundi maarufu kwa jina la Panya Road lavamia maduka, lanyang'anya watu mali zao External Ubungo, Dar leo usiku. Katika taharuki hilo watu walionekana wakihamaki na kukimbia huku na kule ilimradi kila mtu ni kuepusha maisha yake! Habari zaidi bado repota wetu anazifuatilia.....

Wednesday, December 31, 2014

MTUHUMIWA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI MAHAKAMANI

Mtuhumiwa wa kesi ya madawa ya kulevya leo majira ya asubuhi aliuwawa kwa kupigwa risasi na askari magereza baada ya kushindwa katika jaribio la kutoka kutoroka. Mtuhumiwa huyo akiwa amefikishwa mahakamani kutoka mahabusu aliwakimbia walizi hao na kuparamia ukuta wa mahakama akiwa na lengo la kutoroka kabla ya kuuwawa na askari hao waliokuwepo mahakamani hapo. Picha zaidi na wadau wetu. Baadhi ya picha kwa hisani ya Global Publishers

Sunday, December 7, 2014

MDAU WENU NILIPOTEMBELEA MOJA YA MAAJABU 7 YA DUNIA KASRI YA TAJ MAHAL NCHINI INDIA

Mdau wenu nilipokuwa dhiarani nchini India, moja ya maeneo niliyofanikiwa kuyatembelea ilikuwa ni pamoja na makumbusho ya Kasir ya mfalme wa zamani aliyewahi kutawala nchini India. Kivutio kikubwa katika kasri hiyo kubwa iliyosheheni vito vya thamani ni makaburi mawili makubwa ya mke wa tatu wa mfalme huyo pamoja na kaburi la mwanae. Inasemekana mfalme huyo aliyejaliwa kuwa na wake watatu alimpenda sana mke wake wa tatu na hata kuamua kumjengea kasri hiyo ili atakapokufa mwili wake uhifadhiwe humo. Kasri hiyo iliyojengwa na watumishi wapatao 1400 ilikamilika katika kipindi cha miaka 4 na kila mfanyakazi aliyehusika katika ujenzi huo baada ya kumalizika kwa ujenzi mfalme aliamuru akatwe kiganja cha mkono wa kulia kusudi wasiweze kujenga mfano wa kasri hiyo popote hapa duniani. Kasri hii kubwa nchini India ni moja kati ya maajabu saba ya Dunia.
Sanamu ya mfano wa Kasri ya Taj Mahal
Raia mbalimbali wa Kigeni wakiangalia moja ya maajab ya dunia ya Taj Mahal nchin India
 
Mdau nikiwa mbele ya Kasri ya Taj Mahal 
Kila anaefika mahali hapa anapenda kupiga picha ya muonekano huu
 

Thursday, November 20, 2014

AJALI YAFUNGA BARABARA MIKUMI

Leo ama una safari ya kwenda Iringa, Mbeya au kama unapokwenda utapita mikumi basi sitisha safari kwani njia imefungwa tangu saa mbili asubuhi. Kuna lory linawaka moto mpaka sasa. Lilikuwa limebeba lami so lami bado inawaka na imesambaa sehemu kubwa.

Friday, November 14, 2014

BREAKING NEWS!! MACHINGA COMPLEX YAUNGUA MOTO

Soko kubwa na la kisasa lililopo maenea ya Ilala karibu na uwanja wa mpira wa Karume maarufu kama Machinga Complex linalomolikiwa na Manispaa ya Jiji la Ilala katika Mkoa wa Dar-es-Salaam, leo limeteketea vibaya na moto ulioanzia katika ghorofa ya pili. Mpaka tunapata habari hii chanzo cha moto huo kilikuwa hakijajulikana.

Thursday, November 13, 2014

MAJIBU YA SMS KWA MPENZI WAKO VYENYE VIASHILIA VYA KUOMBWA HELA

Ukiona umemtumia mpenzi wako/mchumba wako/mchepuko wako/mke wako au hata rafiki wa kike wakati mwingine SMS ya kawaida tu kwaajili ya kumsalimia lakini yeye akakujibu moja kati ya majibu yafuatayo, tafadhali sana usiendelee kuchat nae maana kinachofuata hapo ni majanga tu.

KWA MFANO: 
1. Ukimtumia sms ''Mambo mpenzi wangu?'' akikujibu ''mambo mabaya'', usimuulize kwanini mambo mabaya, ukimuuliza atakwambia kuwa ''sina hela dear''

2. Ukimtumia sms ''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' akikujibu ''maisha magumu hubby wangu we acha tu'' usimuulize kwanini, ukimuuliza kwanini atakwambia ''nimefulia mwenzio kama nini sijui''

3. Ukimtumia sms ''Mbona kimya sana mchumba wangu, umenitupa kiasi hicho'' akikujibu ''sijakutupa wangu yaani mambo hata hayaendi'' usimuulize kwanini mambo hayaendi, ukimuuliza atakwambia kuwa ''yaani sina kitu mpenzi wangu, simu ilikuwa haina hata hela ya kubeep''

4. Au ukiona mwanamke anaanza kwa kukwambia nikwambie kitu? We mkatalie kiutani utani tu, mwambie usiniambie, hata akikomaa vipi akwambie mwambie sitaki uniambie huku unafanya kama utani lakini moyoni unakuwa upo serious.

Ni mara chache sana mwanamke akikwambia kuwa mambo mabaya, maisha magumu au mambo hayaendi huwa na matatizo mengine kama kuumwa, misiba.... n.k lakini THE REST ni wapigaji mizinga tu. Akikwambia maisha magumu mjibu ''pole wangu, mambo mengine vipi?''

Ukipewa majibu kama hayo, chagua moja, either usiendelee kuchat nae mpaka badae kidogo au mbadilishie maada ili kukwepa huo mzinga ambao unakuja mbele yako. ��������

Thursday, November 6, 2014

MWANAMKE ATUPA KITOTO KICHANGA CHOONI

IRINGA,
Mama mmoja mjini Iringa aamua kumtupa mtoto wake chooni mara baada ya kumzaa nyumbani.
Mtoto huyo wa kiume aliezaliwa tarehe 4/11/2014 majira ya jioni na mama huyo na kuamua kumdumbukiza chooni ambapo kisa mpaka sasa anamkwepa mumewe aliyepo safarin asijue kuwa amepata mimba na kuzaa.
Hata hivyo chanzo cha habari kinasema kuwa, mama huyo kwa jina la magdalena limano (32) mkazi wa Iringa anatabia ya kumdanganya mumewe na kutoka na mabwana wengine pindi mumewe akiwa safarini kikazi.
Mtoto huyo aliyetupwa choon majira ya jioni mara baada ya kuzaliwa na kukutwa asubuhi ya tarehe 5/11 asubuhi akiwa analia ndani ya choo na majirani na kutoa taarifa.
Mpaka sasa mtoto ni mzima wa afya na yupo katika uangalizi mzuri wa hospitali huku mama akishikiliwa na jeshi la polisi akisubiri kupandishwa mahakamani.
Picha zifuatayo linaonyesha tukio kamili: Habari kwa hisani za mtandao wa kijamii Whatsapp.

 
 Kichanga kikisafishwa mara baada ya kuopolewa chooni...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi wa wakuu wapya wanne wa Mikoa, amewahamisha wengine sita na ameamua kuwa wengine watatu watapangiwa kazi nyingine.

Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jioni ya leo, Jumatano, Novemba 5, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa, Wakuu wapya wa Mikoa ni Bi. Halima Omari Dendego ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Dkt. Ibrahim Hamisi Msengi ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Bi. Amina Juma Masenza ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Bwana John Vianney Mongella ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Taarifa inasema kuwa kabla ya uteuzi wake Bi. Dendego alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dkt. Msengi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Bi. Masenza alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela na Bwana Mongella alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.

Taarifa hiyo inasema kuwa Wakuu hao wapya wa Mikoa wataapishwa kesho, Alhamisi, Novemba 6, 2014 saa saba mchana, Ikulu, Dar es Salaam.

Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ambao watapangiwa kazi nyingine ni Kanali (Mst) Fabian Massawe wa Kagera, Dkt. Christine Ishengoma wa Iringa na Kanali Joseph Simbakalia wa Mtwara.

Wakuu wa Mikoa ambao wamehamishwa vituo vya kazi ni Bwana Magesa S. Mulongo ambaye anakwenda Mkoa wa Mwanza kutoka Arusha, Dkt. Rehema Nchimbi ambaye anakwenda Mkoa wa Njombe kutoka Dodoma, Bwana Ludovick John Mwananzila anakwenda Tabora kutoka Lindi, Kepteni (Mst) Anseri Msangi anayekwenda Mkoa wa Mara kutoka Njombe na Mhandisi Everist Ndikilo ambaye anakwenda Arusha kutoka Mwanza.

Wengine waliohamishwa ni Luteni (Mst) Chiku A.S. Galawa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutoka Tanga, Dkt. Rajab Rutengwe ambaye anakwenda Mkoa wa Tanga kutoka Katavi, Bi Fatma Mwasa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kutoka Tabora na Bwana Magalula S. Magalula ambaye anahamishiwa Lindi kutoka Geita.

Taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ya Dar es Salaam, Kigoma, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,Morogoro, Pwani, Rukwa, Shinyanga, Ruvuma, Singida na Simiyu watabakia kwenye vituo vyao vya sasa.

Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi wa Wakuu wapya wa Wilaya, kuhamisha baadhi yao na kutengua uteuzi wa baadhi.

Taarifa kamili itatolewa na Waziri Mkuu baada ya kuwa wamepangiwa vituo vya kazi.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
05 Novemba,2014