Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Wednesday, December 31, 2014

MTUHUMIWA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI MAHAKAMANI

Mtuhumiwa wa kesi ya madawa ya kulevya leo majira ya asubuhi aliuwawa kwa kupigwa risasi na askari magereza baada ya kushindwa katika jaribio la kutoka kutoroka. Mtuhumiwa huyo akiwa amefikishwa mahakamani kutoka mahabusu aliwakimbia walizi hao na kuparamia ukuta wa mahakama akiwa na lengo la kutoroka kabla ya kuuwawa na askari hao waliokuwepo mahakamani hapo. Picha zaidi na wadau wetu. Baadhi ya picha kwa hisani ya Global Publishers

Sunday, December 7, 2014

MDAU WENU NILIPOTEMBELEA MOJA YA MAAJABU 7 YA DUNIA KASRI YA TAJ MAHAL NCHINI INDIA

Mdau wenu nilipokuwa dhiarani nchini India, moja ya maeneo niliyofanikiwa kuyatembelea ilikuwa ni pamoja na makumbusho ya Kasir ya mfalme wa zamani aliyewahi kutawala nchini India. Kivutio kikubwa katika kasri hiyo kubwa iliyosheheni vito vya thamani ni makaburi mawili makubwa ya mke wa tatu wa mfalme huyo pamoja na kaburi la mwanae. Inasemekana mfalme huyo aliyejaliwa kuwa na wake watatu alimpenda sana mke wake wa tatu na hata kuamua kumjengea kasri hiyo ili atakapokufa mwili wake uhifadhiwe humo. Kasri hiyo iliyojengwa na watumishi wapatao 1400 ilikamilika katika kipindi cha miaka 4 na kila mfanyakazi aliyehusika katika ujenzi huo baada ya kumalizika kwa ujenzi mfalme aliamuru akatwe kiganja cha mkono wa kulia kusudi wasiweze kujenga mfano wa kasri hiyo popote hapa duniani. Kasri hii kubwa nchini India ni moja kati ya maajabu saba ya Dunia.
Sanamu ya mfano wa Kasri ya Taj Mahal
Raia mbalimbali wa Kigeni wakiangalia moja ya maajab ya dunia ya Taj Mahal nchin India
 
Mdau nikiwa mbele ya Kasri ya Taj Mahal 
Kila anaefika mahali hapa anapenda kupiga picha ya muonekano huu