Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Tuesday, November 29, 2011

Babuuuuu wa Loliondo!

MTAJI WA JERO JERO KIKOMBE WAMTAJILISHA BABU AMBILIKILE MWASAPILE
MCHUNGAJI Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapile ‘Babu Ambi’ (pichani), anaendelea kusakamwa na wagonjwa wanaodai hawakuponyeshwa na dawa yake, wapo walioweka nia ya kumburuza mahakamani lakini mpya ni pendekezo la kumfilisi.
 Babu Ambi Mwasapile akiwa nje ya nyuma yake ya kisasa.
 Babu akiwa na mjukuu wake mbele ya gari alilonunua kutokana na makusanyo ya dawa ya kikombe aina ya Land Cruser Mkonge.
 Mtambo wa Umeme unaotumia mionzi ya jua unaotumiwa na babu Ambilikile. Hajui matatizo ya Tanesco.
Babu akiwa sebuleni na nyumba full tiles! Je waliowahi kufika loliondo mnakumbuka kile kijumba chake cha chumba kimoja cha udongo? Kweli Mungu amemshushia miujija babu ambilikile! Aaaaaah babuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!

Monday, November 28, 2011

RIP Garry Speed...!

KOCHA WA TIMU YA TAIFA YA WAILES NA MCHEZAJI WA ZAMANI WA NEWCASTLE YA UINGEREZA AJINYONGA
KOCHA wa timu ya taifa ya Wales, Gary Speed amefariki dunia baada ya mwili wake kukutwa ukiwa unaning’inia nyumbani kwake.

Chama cha Soka cha Wales (FAW) kimethibitisha kutokea kwa kifo hicho cha kocha huyo mwenye umri wa miaka 42, ambaye pia aliwahi kuzichezea klabu za Leeds, Newcastle, Everton, Bolton Wanderers  na Sheffield United.