Advert


java

Connectify - Turn Your PC into a Wi-Fi Hotspot. Install now!

Thursday, January 27, 2011

BONANZA LA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA LAFANA LEADERS CLUB

Bonanza la Michezo la lililofanywa na wafanyakazi wa Wizara ya viwanda katika kuukaribishaMwaka mpya lilikuwa ni la kufana na kupendeza.

Wafanyakazi wakicheza mpira wa pete.

Wafanyakazi hapa wakishindana kuvuta kamba.

Mechi kali kati ya timu ya Management na Viwanda Sports Club.


Kina mama nao wakishindana riadha!

Na ukawadia wakati wa kusakata Rhumba.



Wednesday, January 26, 2011

UTAJILI WA SULTAN WA NCHI YA BRUNEI UNATISHA


                              Brunei's Sultan Hassanal Bolkiah
Kasri la Kifahali la mfalme.


Chumba cha Mfalme na mapambo ya dhahabu


Bafu na Masinki ya Kunawia yaliyonakishiwa kwa dhahabu


Ndani ya Ndege ya mfalme wa Brunei.


Chumba cha ndege



Ndege ya Mfalme wa Brunei inavyoonekana kwa nje.


Gari la Harusi ya mtoto wa Mfalme


Choo cha Mfalme


Tuesday, January 25, 2011

CHELSEA YAFANYA MAUAJI

                    Didier Drogba wa Chelsea akilalamika 

Timu ya Chelsea jana iliibuka kidedea kwa kuikamdamiza Bolton kwa magoli 4-0 yaliyofungwa na Drogda, Ramirez,Anelka na Malouda.

SHEREHE YA WANAFAMILIA WA BENKI YA CRDB YAFANA

Shereha ya wana familia wa Benki ya CRDB  iliyofanyika Uwanja wa maji  kunduchi siku ya Jumapili.




 Wafanyakazi wa CRDB wakipozi kwa Picha.
 




 Watoto wa wanafamilia nao walikuwepo.


Wadau wakiwa na Mascot katika kusherehesha

 Vivywaji vilikuwa vya kutosha.

Wafanyakazi na wadau wa Benki ya CRDB walioudhuria sherehe hiyo ya wanafamilia wakidualika.

Tuesday, January 18, 2011

MTANZANIA ATUNUKIWA TUZO NA MALKIA WA UINGEREZA

                         Charity supporter and IT chief, Ashok J Rabheru

Mtanzania Ashok Rhaberu aliyezaliwa katika mji kasoro bahari Mkoa wa Morogoro mwaka 1952 amefanikiwa kutunukiwa tuzo ya juu ya CVO (Commander of Victorian Order)na Malkia Elizabeth wa II katika sherehe za kuukaribisha mwaka mpya.

Rhaberu ambaye ni mmoja wa kundi la wafanyabiashara wa Tanzania waliopo Uingereza (Tanzanian-UK Group) anamiliki asasi isiyo ya kiserikali inayosaidia maendeleo ya Tanzania.

Saturday, January 8, 2011

KOCHA WA LIVERPOOL ABWAGA MZIGO

Kocha wa timu ya Liverpool Roy Hudgson.

Kocha wa timu ya Liverpool Roy Hodgson amebwaga manyanga na kuacha kuifundisha timu ya Liverpool baada ya kufanya vibaya katika Ligi kuu ya Uingereza inayoendelea huku timu hiyo ikishika nafasi ya 12 katika msimamo wa lIgi.

Kocha huyo anaachia ngazi huku akiwa ameiongoza klabu hiyo kwa takribani miezi saba tu. Kwa sasa timu hiyo itaongozwa na Kocha Kenny Daglish aliyewahi kukipiga katika timu hiyo inayojulikana kama majogoo.

Thursday, January 6, 2011

MAANDAMANO NA VURUGU ZA KISIASA ARUSHA

Viongozi wa CHADEMA wakishirikiana na wanachama wao katika maandamano mjini Arusha leo

 Wanachama wa CHADEMA wakizuiwa na Askali wa kutuliza ghasia.
 Wanachama wa CHADEMA wakitaka kuandamana kwa amani.
 Mabomu ya machozi yakipigwa na FFU kutawanya waandamanaji.

 Jiji la Arusha likijaa moshi wa machozi kwa aliyekuwemi na asiyekuwemo.

         Askali wa kikosi cha FFU wakitanda barabarani kwa doria

                    Magari ya askali yakiwa mitaani

 Raia wema na wapita njia wakibubujikwa na machozi kutokana na mabomu

  Mke wa Katibu mkuu wa CHADEMA akivuja damu baada ya kupigwa na Askali
                     Akijisalimisha kwa Askali wa FFU.

        Askali wakijaribu kutaka kuendelea kumwadhibu

Mke wa katibu mkuu wa Chadema Dr. Slaa wa CHADEMA akivuja damu baada ya kujeruhiwa katika vulugu zilizotokea katika maandamano hayo.

Habari zilizomfikia kaka zinasema Katibu Mkuu wa chama hicho Dr. Slaa na Mbunge wa Arusha Mh. Ndesamburo wametiwa mbaroni kutokana na vurugu hizo! Je kulikuwa hakuna njia mbadala ya kutuliza maandamano bila ya kipigo? Je maandamano hayo hayakuwa ya amani???

Wednesday, January 5, 2011

BENDI YA MAPACHA WATATU YAREKODI VIDEO YA SINGLE YAO YA MUHUDU

     Mapacha watatu wakifanya shooting ya Video

Bendi ya Mapacha watatu inayoundwa na Kharid Chokoraa, Jose Mara Na Kalala Junior leo walionekana wakifanya shooting ya single yao mpya inayojulikana kwa jina la Muhudu katika maeneo ya Sneak Peak. Haya wadau tuisubili kwa hamu single hiyo katika Luninga zetu tuone jinsi wazee walivyokandamiza......

DUH! UBUNIFU WA KUCHAKACHUA





                          Jamaa akiwa ndani ya Usafiri wake

Katika hali ya kufurahisha kaka nilipita mitaa fulani wanakotoka kina Niangusage Mwenyewe na kukuta ubunifu wa hali ya juu ambapo jamaa huyu alichakachua kichwa cha lori aina ya FIAT kuwa  nusu gari lililokuwa likikokotwa na Ng'ombe. Gari hilo lina uwezo wa kubeba abilia na dereva akiwa sehemu inayokaa Injini! Wabongo kweli wanatisha kwa uchakachuaji.

MICHANGO MIKUBWA YA SHEREHE INA ULAZIMA?

                                  Maharusi wakiwa katika honeymoon.

Nimekuwa nafuatilia jinsi desturi ya kuchangia na kufanya sherehe kubwa
inavyozidi kushika kasi, ikipelekea ule wigo wa kuomba michango kupanuka
kiasi kwamba sasa hata mtu ambaye jina lako halijui vizuri anaweza kukuomba
mchango.


Aidha michango na sherehe hizi zimekuwa mzigo mkubwa sana kwa baadhi ya
watu, ikiwa ni pamoja na wale wenye kipato kidogo wanaochangiwa na
kulazimika kulipa michango hiyo kwa miaka mingi. Je, wajua kuwa kuna familia
ambazo zimefikia kulazimisha ndugu wauze mashamba au mifugo mtaji ili kupata
fedha za kuchangia sherehe?. Je, wajua kuwa kuna watu ambao zaidi ya nusu ya
kipato chao wanatumia kuchangia sherehe na huku wakishindwa kulipia huduma
muhimu kama shule, matibabu, lishe, nk. Na kuwa wakati mwingine wewe au mimi
(au wengine kama mimi na wewe) ndio wenyeviti na makatibu wa sherehe hiyo?.
Na ni sisi tunaoona fahari ya kutumia milioni 30 au zaidi kwenye sherehe
usiku mmoja?


Kuna kijana mmoja jamaa yetu juzi juzi alipata shule Australia akawa
anatafuta mchango wa dola 5,000 aende. Alipata 2,000 na amwekwama kwenda.
Mwaka kesho akisema anaoa tutamchangia milioni 15-20!!!. Hii si hadithi, ni
ukweli, na ni kielelezo cha ulimbukeni tuliofikia.


Siku za karibuni nimetambua kuwa kuna kundi kubwa tu linasikitishwa na huu
mwenendo, na hata kutambua kuwa tunaweza kuwa tunaandikiwa dhambi kubwa (na
hukumu yatusubiri) kwa jinsi wengi wetu tunashindwa kusaidia mambo ya msingi
lakini tunakuwa wepesi kutoa kwenye sherehe. Wengi wanaamini kuwa
tumeshatumbukia kwenye lindi la mazoea ambapo hatuwezi kujitoa mpaka upepo
uje ubadilike wenyewe!.


Mimi nafikiri wasomi tuna jukumu muhimu la kuwa chachu ya mabadiliko pale
ambapo mazoea yenye madhara yanavuka mipaka na kuweza hata kuwa chanzo cha
ufukara na kuviza maendeleo.


Ili kubadilisha hili jambo, lazima tuanzie mahali. Mimi napendeleza na
kuanza kutekeleza. Kuanzia Januari 2011, nitapunguza michango ninayotoa.
Nitatoa tu kwa mtu wa karibu sana, na nitachanga kidogo. Usishangae
nikakuchangia 20,000/= kama ulitegemea 50,000/= kwa mfano. Kuanzia July
2011, nitaacha kabisa kuchangia sherehe. Badala yake nitakuwa nachangia
elimu pale ambapo mzazi hayupo au mhusika kweli hana uwezo na pia
nitachangia miradi mingine ya jamii na maendeleo.


Je waniunga mkono? Kama ndiyo sambaza huu ujumbe kwa mtandao wako.

Tuesday, January 4, 2011

KARIBUNI

Napenda kuwakaribisha wadau wote wa habari motomoto katika Blog hii inayofunza na kuburudisha wakati wote utakaokuwa unaperuzi habari zilizomo humu. Karibuni sana nyote. Aksanteni.